Wednesday, May 21, 2014

WAZIRI MUKANGARA AONGOZA MAELFU YA WATANZANIA KUTOA HESHIMA ZA MWISHO KWA MWILI WA MAREHEMU ADAM KUAMBIANA

Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akitoa heshima za mwishomapema hii jana katika viwanja vya Leaders kwa mwili wa msanii wa Filamu nchini Marehemu Adam Philip Kuambiana aliyefariki ghafla mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam.
Mjane wa marehemu Adam Kuambiana, Bi. Janeth Rite akiwa katika wakati mgumu kutokana na kushuhudia mwili wa mme wake ukiwa katika jeneza.
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Serikali, kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki wa marehemu Adam Philip Kuambiana wakati wa shughuli za kutoa heshima za mwisho kwa marehemu iliyofanyika leo katika viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam, kushoto ni mjane wa marehemu Bi. Janeth Rite.
Katibu Mtendaji wa Bodi ya Ukaguzi wa Filamu Tanzania Bi. Joyce Fisso akitoa salamu za rambirambi kwa niaba ya Bodi ya Filamu kwa familia ya marehemu Adamu PhilipKuambiana aliyekuwa msanii wa Filamu na mkurugenzi wa Kampuni ya kutengeneza filamu ya APK akiyefariki ghafla siku ya jumamosi kutokana na ugonjwa wa Vidonda vya Tumbo.
Mstahiki Meya wa Manispaa ya Kinondoni Yusuf Mwenda akitoa salaam za rambirambi kwa niaba ya Manispaa ya Kinondoni ambapo mjane wa marehemu Adam Kuambiana anafanyakazi kama Diwani wa Kata ya Kunduchi. ,kushoto katikati ni Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Fenella Mukangara na mjane wa marehemu Mhe. Janeth Rite
Msanii wa Muziki wa injili na Bongo Flava Stara Thomas akiimba kwa hisia wakati wa shughuli ya kutoa heshi za mwisho kwa mwili wa marehemu Adam Kuambiana jana katika viwanja vya leaders jijini Dar es Salaam.
Mwenyekiti wa Bongo Movie Steve Mengere maarufu kama Steve Nyerere akitoa salaam za rambirambi kwa niaba ya Bongo Movie wakati wa shughuli za kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Adam Philip Kuambiana.
Msanii wa Filamu Jacob Steven – JB akitoa maelezo kuhusu umuhimu wa marehemu Adam Kuambiana katika tasnia ya Filamu nchini,katika maelezo yake JB amesema kuwa Adam alikuwa injini katika sanaa ya filamu hivyo ni pengo kubwa ambalo hajui litazibika namna gani.
Msanii wa Filamu nchini Wema Isack Sepetu akiwa katika majonzi makubwa wakati wa shughuli za kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa msanii mwenzake marehemu Adam Philip Kuambiana iliyofanyika katika viwanja vya Leaders jana jijini Dar es Salaam.

Baadhi ya wananchi waliohudhuria shughuli za kutoa heshima za mwisho kwa mwili wa marehemu Adam Kuambiana wakiwa katika taswira mbalimbali. 
Picha zote na Frank Shija, Afisa Mawasiliano Serikalini-WHVUM

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI