Wednesday, May 21, 2014

BRENDAN RODGERS ACHEKELEA KUPAMBANA NA VAN GAAL WA MAN UNITED MSIMU UJAO

KOCHA wa Liverpool, Brendan Rodgers amefurahia kujipima uwezo na moja ya makocha wakubwa duniani, Louis van Gaal anayetarajia kuiongoza Manchester United msimu ujao.
Mholanzi huyo alitangazwa kurithi mikoba ya David Moyes jumatatu ya wiki hii kwa lengo la kurudisha hadhi ya Man United, na kocha Rodgers anaona ni chaguo sahihi kwa mashetani wekundu.
Rodgers amemfurahia Van Gaal, lakini amesema Moyes hakupewa muda zaidi wa kufanya makubwa Old Trafford.
“Kwanza kabisa, ilihuzunisha kuona Moyes hakupewa fursa ya kutosha,”. Kocha huyo wa Liverpool aliwaambia talkSPORT.
Van Gaal
“Moyes aliondoka na kwa vyovyote vile walihitaji kutafuta kocha mwingine na wameona Van Gaal anastahili. Hata mimi nakubali, ni mtu niliyejifunza kutoka kwake kwa miaka mingi”. Alisema Rodgers.
“Ana mafanikio makubwa, ni mtu mwenye maono makubwa na ana njia zake za kuona mpira unachezwa. Anafanya kazi na wachezaji vijana. Nadhani ataifaa Manchester United”.
“Nikiwa kocha kijana, nafurahi sana kushindana na kocha mkubwa katika ulimwengu wa soka”.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI