Tuesday, May 20, 2014

BENKI YA CRDB YATOA MSAADA WA MILIONI 10 KWA SHULE YA SEKONDARI YA WASICHANA KIBOSHO

Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akisaini kitabu cha wageni alipofika katika Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Kibosho, wakati wa mahafali ya Kidato cha Sita. Kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya Shule, Mhandisi Aloyce Peter Mushi. 
Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Kibosho, Sista Anna akimpeana mkono na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei wakati wa mahafali ya Kidato cha sita yaliyofanyika Shuleni hapo. Benki ya CRDB ilitoa msaada wa shs. milioni 5 na katika harambee iliyofanyika shuleni hapo jumla ya sh.milioni 10 zilipatikana. 
Baadhi ya wahitimu wa Kidato cha Sita wakiimba ngojera wakati wa sherehe za mahafali ya kidato cha sita.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akiwasili Shuleni hapo.
Mkuu wa Shule ya wasichana ya Kibosho, Sista Anna akizungumza wakati wa mahafali hayo.
Mwenyekiti wa Bodi ya Shule ya Sekondari Kibosho, Mhandisi Aloyce Peter Mushi akizungumza wakati wa hafla ya mahafali ya Kidato cha Sita ya Shule ya Sekondari ya Kibosho. Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki
ya CRDB, Dk. Charles Kimei 
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dk. Charles Kimei akizindua jengo la mahabara ya Shule ya Sekondari
Kibosho, wakati wa mahafali ya 30 ya kidato cha sita yaliyofanyika Mkoani Kilimanjaro. Kushoto ni Mkuu wa Shule hiyo, sista Anna na kulia ni Mwenyekiti wa Bodi ya shule hiyo, Mhandisi Aloyce Peter Mushi. Benki ya CRDB ilitoa mchango wa shs. milioni 5 kwa ajili ya shule hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk. Charles Kimei akipata maelezo kutoka kwa Mwenyekiti wa Bodi ya Shule, Mhandisi Aloyce Peter Mushi. Kulia ni Mkuu wa Shule hiyo, Sista Anna. 
Shule ya Serkondari ya Kibosho.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dk. Charles Kimei akizindua gazeti la shule. Kushoto ni Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Kibosho, Sista Anna na Mwenyekiti wa Bodi ya Shule, Mhandisi Aloyce Peter Mushi.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI