Thursday, April 10, 2014

BREAKING NEEEWZZZ!!! MGAMBO WA OPERESHENI SAFISHA JIJI WAVUNJA MAKABURI YA SHEIKH YAHYA NA SHEIKH KASSIM

 Habari zilizotufikia hivi punde zinasema kuwa Mgambo wa jiji wanaoendelea na Operesheni ya safisha jiji kwa kuwaondoa wafanyabiasha wadogo na wauza magazeti katika maeneo yasiyo rasmi, muda huu wamevamia makaburi ya Sheikh Kasim Bin Juma na Sheikh Yahya Hussein, yaliyopo eneo la makaburi ya Tambaza jirani na Muhimbili na kuyavunja.  Haikuweza kufahamika haraka kuwa makaburi hayo ni miongoni mwa uchafu wanaoshugulikia kuuondoa ama vipi.
  
 Baadhi ya wananchi ndugu na jamaa wa marehemu waliolala kwenye makaburi hayo waliofika kushuhudia mgambo hao wasiotaka kusikia la mtu.
 Mwandishi wa Itv, Godfrey Monyo, akiwa eneo la tukio.
 Haya ni baadhi ya majengo ya katikati ya mji yaliyobomolewa na mgambi hao.
 Paa la moja ya jengo lililobomolewa.
 Mapaa yote yaliyoongezwa katika majengo yalibomolewa.
 Hali ya baadhi ya majengo katikati ya mji ni kama hivi.
 Haya yote yamebomolewa.....
Kazi inaendelea......

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI