Monday, October 19, 2015

TANZANIA YAINGIA KWENYE RAMANI YA FILAMU DUNIANI BAADA YA USHINDI WA TUZO YA MTANZANIA MWINGINE CALIFORNIA MAREKANI 2015

Kutana na Timoth Conrad Kachumia ‘Tico’, mtanzania ambaye nguvu zake, akili yake na utundu wake siku zote ameuelekeza kwenye utengenezaji wa filamu za Kitanzania akiwa kama ‘muongozaji na muandaaji’
timoth conrad 3
Timoth ameipa Tanzania headlines kwenye tuzo za SILICON VALLEY AFRICAN FILM FESTIVAL ambazo zimekua zikifanyika kila mwaka California, Marekani kwa kushinda tuzo moja ya ‘Achievement in Narrative Feature Film‘ iliyokuwa ikiwaniwa na nchi 9 za Afrika.
timoth conrad 4
Kwenye exclusive interview na reporter wako Millard Ayo aliyeko hapa Marekani, Timoth amesema ‘kwenye hicho kipengele nilikua nashindana na Ghana, South Africa, Nigeria, huu ni wakati wa Watanzania kuamka na kufanya kazi nyingi nzuri zaidi, huu ushindi sio kitu kidogo upinzani ulikua mkubwa’
Timoth Conrad 1
‘Tumekubalika sana… hii filamu yangu inawazungumzia watoto watatu waliokua wakitafutwa na viumbe vingine kutoka sayari nyingine, sio stori ya kweli ila ni ya kufikirika… ni stori ambayo niliiandika mwenyewe’ – Timoth
timoth conrad 4
#Milladayo.com

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI