Tuesday, April 15, 2014

ANGALIA PICHA ZA SIMBA ALIYEJERUHIWA NA NYATI KWEUPE PEEH!

Picha linaanza hivi: Bibi Simba yupo kwenye mawindo yake kama kawaida, anajitafutia riziki, anamuona yati jike akikatiza anamnyatia kama kawa, anafanikiwa kumdondosha.. ile anataka kumaliza mchezo, Nyati dume linatokea na kumtupa juu juu Bibi. Simba, ambaye anajeruhiwa vibaya kama anavyoonekana hapa chini akitafuta sehemu ya kupumzika kwa uchovu alioupata. 

Alipopata sehemu ya kujipumzisha akabaki kuuguza donda lake jipya na kubaki akijilaumu kuwa kwanini asingebaki tu kulala kama walivyo wenzie.
Simba huyu alipata bahati kwani alipata huduma nzuri toka kwa madaktari wa wanzama katika mbuga hizo na hatimaye kupona kabisa, nahisi hakutamani tena nyama ya Nyati kwa siku hiyo kabisaaaaaa! Pole Bibi. Simba.









Safari inaendelea, sasa sijui kama bado ana nguvu tena ya kumuua nyati au anatafuta Swala a.k.a Take away!

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI