Monday, September 7, 2015

LOWASSA "AITIKISA" DAR, MBEZI YATAPIKA PEOPLE'S....WAMWAMBIA "ULIPO TUPO" *PICHAZ*

 
Mh. Lowassa na viongozi wengine wa UKAWA, wakiwa jukwaani mbele ya umati wa watu
Wananchi wakionyesha alama ya mabadiliko inayotumiwa hivi sasa na UKAWA
Mh. Lowassa, na Mwenyekitin wa CHADEMA, Mh. Mbowe, wakiwasili kwenye eneo la mkutano huko Kibamba
Mgombea kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia vyama vinavyounda UKAWA, Mh. Edward Lowassa, September 07, 2015 amelitikisa jiji la Dar es Salaam, hususan maeneo ya Kibamba kulikofanyika mkutano wa kihistoria wa kampeni ambapo maelfu ya wananchi walifurika wengine wakikaa juu ya mapaa ya nyumba za madarasa, wengine kwenye miti, kutokana na kukosa eneo zuri la kuweza kushuhudia "live" mkutano ukiendelea. Changamoto ya maeneo ya kufanyia mikutano ya kampeni ndiyo inayoonekana kuikumba UKAWA, kutokana na kuongezeka kwa idadi ya watu wanaohudhuria mikutano hiyo.
Pichani mfuasi wa UKAWA, akiwa amejichora rangi za bendera ya CHADEMA akiambatanisha maneno maarufu yanayotumiwa na wafuasi wa Mh. Lowassa kwa sasa, yaani "Ulipo tupo".

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI