MSANII wa Muziki wa Bongo Fleva Juma Nature jana ameongea na Waandishi wa Habari juu ya Ufanyaji kazi wake katika kipindi hiki cha kampeni Ambapo aliongozana na Mgombea Ubunge jimbo la Mbagala ambaye ni rafiki mkubwa na jirani wa msanii huyo Ndg Issa Mangungu.
Juma nature kwa sasa amerudi kufanya kampeni na chama cha mapinduzi CCM na ameamua kuelezea nia ya kurudi CCM baada ya mashabiki kumuona katika Majukwaa mengine ya vyama vya kisiasa.
Nature amesema kuwa mziki ambao anaufanya ni Biashara lakini pia anafanya kwa ajili ya Jamii yake ambayo inamzuuka na pia anaangalia sehem ambayo anakubalika ivyo akiitwa sehem yeyote kufanya kazi anaenda anafanya kazi maana mziki ndio ajira yake.
Sikilize hapa Juma Nature akiongea…….