Friday, October 17, 2014

MAKUBWAAA!!! MISS TANZANIA 2013 AMSHAURI SITTI MTEMVU KURUDISHA TAJI.. SOMA ALICHOSEMA HAPA!

KAMA na wewe unakerwa au haupendi jinsi ambavyo Miss Tanzania wa 2014 Sitti Mtemvu amekua akiandamwa kwenye mitandao ya kijamii kuhusu umri wake na elimu yake baada ya kushinda taji hilo weekend iliyopita basi uko upande mmoja na Miss Tanzania wa 2013 Brigitte Alfred.
Kupitia page zake za twitter na Instagram Brigitte pamoja na mengine ameandika >>> ‘Mazuri mengi yanawapita lakini inapotokea skendo mnajadili milele ndio maana hatuendelei, natamani tungeweka hizi nguvu za matusi kwenye vitu vya kujenga

Baada ya hiyo sentensi Brigitte alimuandikia Sitti kwa kusema >>> ‘Sitti usiwaruhusu watu wakuandame sana, ikizidi warudishie tu taji lao’
Kwenye tweets nyingine za wiki hii baada ya Sitti kutangazwa mshindi Brigitte aliandika ‘mngejua siasa za huko Miss World hata msinge jisumbua kumshambulia huyu msichana kiasi hicho, mtihani wa Miss Tanzania sio tu siku ya fainali ndio maana kunakua na camp ya siku 30′ Miss TZ 2
Miss TZ 3

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI