Saturday, September 27, 2014

SANDRA - SIJAWAHI KUTOA RUSHWA YA NGONO KWA DIRECTOR WALA PROMOTA NA SINTOKAA NITOE.. SHUKA NAYO HAPA

MSANII wa siku nyingi katika tansia ya filamu Bongo, Salama Salmin ‘Sandra’ amefunguka kuwa tangu ameanza kujihusisha na mambo ya sanaa hajawahi kuwa na bwana ndani ya klabu ya Bongo Movies na wala hajawahi kutoa rushwa ya ngono kwa ‘dairekta’ kama ilivyo kwa wengine.
Akizungumza na mwandishi wa habari hii hivi karibuni, Sandra alisema kuna baadhi ya wasanii wanafikiri kuwa na mwanaume ndani ya Klabu ya Bongo Movie ndiyo kutimiza ndoto zao kumbe ni kujidharaulisha tu.
“Sina bwana wala sijawahi kutoa rushwa ya ngono kwa ‘dairekta’ na sifikirii kufanya hivyo kamwe, maana ni kujishushia heshima yangu  wakati mimi ni mke wa mtu na wala siwezi  kunadi mwili wangu,” alisema Sandra.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI