Muonekano wa gari hilo lilivyogongwa kwa nyuma.
AJALI imetokea leo mchana maeneo ya njia panda ya Ilala ambapo gari ndogo aina ya Toyota Rav 4 lenye namba za usajili T606 CHH liligongwa na Toyota DCM linalofanya safari zake kati ya Posta na Tabata Kimanga.
Rav 4 ilifunga breki ghafla na basi likagonga kwa nyuma. Hakuna majeruhi wala mtu aliyefariki dunia.
(Habari/Picha na GP)






0 comments:
Post a Comment