Friday, August 8, 2014

AJALI ILYOTOKEA ENEO LA AFRIKANA, MBEZI BEACH

 Gari aina ya Nissan Hard Body yenye Namba za Usajili T 524 ALW likiwa limetupwa mtaroni na trela la lori (halipo pichani) ambalo lililigonga gari hilo na kutumbukia mtaroni eneo la Afrikana Mbezi Beach Mchana tar 07 mwezi huu. 
Katika Ajali hiyo iliyohusisha Lori na gari aina ya Nissan Hard Body hakuna mtu yoyote aliyepoteza Maisha.
 Wananchi wakisaidia Kulifunga minyororo gari aina ya Nissan Hard Body ambayo imetumbukia mtaroni mara baada ya Kugongwa na trela la lori (halipo pichani) mchana wa tar 07 mwezi huu katika Eneo la Mbezi Afrikana
Wananchi wakisaidia kuligeuza gari ndogo aina ya Nissan Hard Body iliyotumbukia mtaroni eneo la Afrikana Mbezi Beach mara baada ya Kugongwa na trela la lori (halipo pichani) mchana wa tar 07 mwezi huu, katika ajali hiyo hakuna aliyepoteza maisha. 
Picha na Lukaza Blog

0 comments:

Post a Comment