Tuesday, July 15, 2014

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI ALIPOTEMBELEA SHIRKA LA NDEGE TANZANIA (ATCL)

Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba (kulia), akisalimiana na Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Mr. Salim Msoma wakati alipotembelea shirika hilo mwishoni mwa wiki iliyopita kuongea na Bodi, Menejiment na wafanyakazi wa Shirika hilo. Nyuma ya Mr Msoma ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa Shirika hilo, Kapteni Milton Lazaro.
Naibu Waziri wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba akisisitiza jambo wakati wa kikao chake na wajumbe wa bodi na menejiment ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), wakati alipoongea nao mwishoni mwa wiki katika ofisi za Makao ya Shirika hilo.
Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba, akisisitiza jambo wakati alipoongea na Bodi, Menejimenti na wafanyakazi wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), Naibu Waziri aliwasisitiza watumishi hao kufanya kazi kwa bidii na kurudisha sifa ya shirika hilo. 
Picha na kitengo cha Mawasiliano Serikalini-Uchukuzi

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI