Tuesday, July 15, 2014

MAN UNITED YAPATA BONGE DILI LA MABILIONI REKODI NZIMA

KLABU ya Manchester United imesaini mkataba wa rekodi wa udhamini wa vifaa vya michezo, wenye thamani ya Pauni Milioni 75 kwa mwaka na Adidas.
Kiwango hicho ni zaidi ya mara mbili ya mile ambacho walikuwa wanaoata kutoka kwa wadhamini wao wa sasa, Nike na Mkataba huo mpya ni wa miaka 10. 
Hiyo inamaanisha watapata Pauni Milioni 750 kwa muongo mmoja, lakini Adidas imesema itapata faida Pauni Bilioni 1.5 kwa mauzo ya jezi katika kipindi hicho.
Onyesho la mwisho: 
Ndoa ya Nike na Manchester United itafikia tamati baada ya msimu ujao
Taarifa ya United imesema: "Manchester United imefikia makubaliano ya miaka 10 na adidas ya udhamini wa vifaa vya michezo wenye thamani ya Pauni Milioni 750, ambayo inaweza kuwa inaongezeka kuanzia msimu wa 2015/2016.'
Mtendaji Mkuu wa Adidas, Herbert Hainer amesema: "Tumefurahia kuungana na Manchester United, moja kati ya klabu zenye mafanikio na zinazopendwa ulimwengun,".
Mkataba wa United unatarajiwa kuanza msimu wa 2015-2016.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI