Tuesday, May 27, 2014

STATUS KATIKA FACEBOOK YA ALICHOKISEMA MAREHEMU RECHO KABLA YA UMAUTI KUMKUTA!

Screen Shot 2014-05-27 at 8.56.46 AM
Tukiwa na wiki moja toka tumzike muongozaji na muigizaji Adam Kuambiana leo asubuhi imetoka taarifa nyingine ya kifo cha miongoni mwa waigizaji wa kike toka Bongo Movie.

Aliefariki ni mwigizaji anaitwa Rachel Haule ambaye kacheza movie mbalimbali ikiwemo Vanesa in Dilema.
Screen Shot 2014-05-27 at 8.56.59 AM
Chanzo cha kifo chake chake bado hakijafahamika ingawa taarifa za mwanzo zinasema alikua mjamzito na alikwenda Muhimbili kwa ajili ya kujifungua baadae alifanikiwa kujifungua lakini kwa bahati mbaya mtoto alifariki nae hali ilibadilika akapelekwa ICU lakini baadae akafariki.
Hii ni status yake ya mwisho Facebook.
Screen Shot 2014-05-27 at 8.56.22 AM
Moja ya waigizaji walioandika kuhusu kifo cha Rachel ni Shilole >>> 
‘sitaki kumkufuru Mugu wangu ila kazi yake haina makosa, tulimpenda ila mwenyenzi Mungu kampenda zaidi, duh.. inauma sana pole Saguda kwa mtihani uliokupata ila tupo pamoja kwa kipindi hiki kigumu'

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI