Tuesday, May 27, 2014

PSI YAFANYA MKUTANO NA WASAMBAZAJI WA KANDA YA KASKAZINI

Shirika lisilo la kiserikali linalo fanya kazi chini ya wizara ya afya PSI/Tanzania kanda ya kaskazini ambalo ni wasambazaji wa salama kondom na bidhaa nyingine za afya zikiwezo zile za uzazi wa mpango za familia pamoja watergurad, mwishoni mwa wiki limefanya mkutano na mawakala wateule wa kanda ya kaskazini inayohusisha mikoa ya Tanga, Kilimanjaro, Arusha an Manyara uliofanyika katika hoteli ya Silver Palm iliyoko hapa jijini Arusha ukiwa na lengo la kujadili mafanikio, changamoto na kuweka mikakakati ya kufanikisha na kuimarisha usambazaji wa bidhaa hizo kwa kanda ya kaskazini.
Akizungumzia hali ya usambazaji wa salama kondom meneja wa usambazaji wa kada ya kaskazini wa PSI Tanzania ndugu Pelestian Masai, amesema mpaka sasa PSI kanda kwa kushikirikiana vema na wadau wake na wamefanikiwa kusambaza salama zaidi ya Kondom milioni 9 katika mikoa hii minne ambapo lengo kwa mwaka huu ni kufikia condom zaidi ya milioni 20, wakati jiji la Arusha pekee kwa mwaka 2014 ndilo linaongoza likiwa limesambaziwa zaidi ya condom milioni 5 kwa mwaka huu pekee.
lengo likiwa ni kusaidia juhudi za serikali katika jitihada za kupambana na mambukizi ya ukimwi, magonjwa ya ngono pamoja na kuboresha huduma za uzazi wa mpango.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI