Friday, March 7, 2014

TAFAKARI: SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

HAKIKA kwa miaka ya hivi karibuni kumekuwa na kauli mbiu ama unawezaita ni mikakati kabambe ya kumuinua mwanamke katika nyanja zote; katika jamii, siasa na zaidi kiuchumi.

Kamwe palipo na ukweli uongo hujitenga kwani ni ukweli usiopingika jamii nyingi za kiafrika zimetawaliwa sana na mfumo dume ambapo umekuwa ukitawala katika nyanja hizo zilizotajwa hapo juu.

Mfumo huo kwa sasa unapungua kwa kiasi kikubwa na ni imani ya waafrika na watanzania wengi mfumo huo upotee na uishe kabisa kwani mwanamke hatokuwa kiumbe dhaifu mbele ya mwanaume na haki, usawa, amani na upendo vitatawala kitu kitakacholeta maendeleo.

TAFAKARI: Ni je wanawake wenyewe wanapendana na kujaliana?

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI