Friday, March 21, 2014

D'BANJ AWAZAWADIA WA-NIGERIA 'KOKO GARI'


MWANAMUZIKI maarufu nchini Nigeria anaetamba na vibao kama vile Fall in love, Don't tell me nonsence, Oliver twist na vingine vingi, ameamua kuzindua biashara yake mpya ya kuuza chakula kiitwacho gari.
Gari ni chakula rahisi sana katika kukitumia kwani ni chakula kitokanacho na mihogo na kinacholiwa kwa kuchanganya na sukari, chakula hiki ni maarufu sana nchini Nigeria, Ghana na nchi karibu za kaskazini mwa Afrika.
D banji amezindua bidhaa hii mpya ijulikanayo kama 'Koko Garri' katika kampeni ijulikanayo kama One Do Agric iliyofanyika katika hotel ya Transcorp Hilton jijini Abuja, Nigeria.
Mwanamuziki huyu ametoa tangazo lake katika mitandao ya kijamii Instagram, Twitter na blog mbalimbali akielezea uzinduzi huo ambapo ametweet akisema "Hatimaye baada ya miaka mitano, naweza sema Koko gari ni bidhaa itokanayo na Koko holdings, Namshukuru Mungu".
Click for Full Image Size
Click for Full Image SizeClick for Full Image Size
Koko Holdings ni kampuni inayomilikiwa na msanii huyu ambapo mwaka 2011 D'banj alikuwa ni mwanamuziki wa kwanza kuzindua simu zake za mkononi alizozipa jina la Koko mobile, lakini hazikufanya vizuri sokoni na hatimaye zikapotea.
Click for Full Image Size
Wasanii wetu wa kitanzania ni imani kuwa wanajifunza kitu toka kwa wasanii kama hawa maarufu ambapo wanajihusisha na kazi nyingine tofauti na muziki ili kujiongezea kipato na kujikwamua katika maisha.

Vizuri tuige, vibaya tuachane navyo! Hongera D'Banj kwa hili mengine mengi mazuri yanayokuja mbele yako.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI