NYUMBANI KITAIFA
Ulimwengu wa habari.
KATIKA BIASHARA
Ulimwengu wa habari.
MATAIFA MENGINE
Ulimwengu wa habari.
KATIKA BURUDANI
Ulimwengu wa habari.
MAAJABU DUNIANI
Ulimwengu wa habari.
Friday, January 11, 2013
JE UNGEPENDA UPATE KALENDAR YAKO MWENYEWE KAMA HII?
9:18 AM
No comments
SERIKALI YALIFUFUA SHIRIKA LA RELI
8:57 AM
No comments
![]() |
| Rais Jakaya Mrisho Kikwete (yumo garini kushoto) akikagua sehemu ya kutua na kupaa ndege ya uwanja wa Tabora Januari 10, 2013 mara baada ya kuzindua rasmi ujenzi wake |
Thursday, January 10, 2013
WASANII WA FILAMU WALIVYONOGESHA UZINDUZI WA KAMPENI YA KILIMO KWANZA KATA YA KWADELO, KONDOA
1:53 PM
No comments
Wasanii wa filamu, kutoka kushoto; Jacob Steven 'J B', Vicent Kigosi 'Ray', Irene Uwoya, Wema Sepetu na Single Mtambalike 'Rich Rich' walipowasili Kwadelo kwa ajili ya kushiri uzinduzi huo wa kampeni ya Kilimo Kwanza kwa vijana wa Kata hiyo.
Wazee wa Kwadelo wakati wakisubiri kuwasili kwa diwani wao pamoja wasanii hao
Baadhi ya akinamama wa Kwadelo waliohudhuria hafla hiyo
Ray akipozi picha na wazee wa Kwadelo
Kariati akiwa na wasanii hao kwenye trekta kabla ya uzinduzi wa kampeni hiyo
Wema Sepetu akiungurumisha trekta ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa kampeni hiyo. Wapili Kulia ni Omary Kariati
Uwoya naye akilijaribu trekta kwenye uzinduzi huo
KWADELO HOYEEEEEE! JB akihamasisha wakati wakiwa kwenye trekta la kilimo katika uzinduzi huo
Treka likionyesha mfano wa ulimaji wa kisasa kwenye shamba la shule ya sekondari ya Kwadelo wakati wa uzinduzi huo
KITUKO: Panzi! Panzi! Panzi!, Wema Sepetu (shati ya kijani) akifunika uso wake kwa kipochi chake, huku akipiga kelele na kujiingiza katika kundi la wazee, kwa sababu ya kuogopa panzi aliyemdandia wakati wa shughuli za uzinduzi huo shambani.
J B na Wema wakila mapozi shambani wakati wakienda sehemu ya uzinduzi
Wema akitangaza kuzindua kampeni hiyo
BAADAYE: Wasanii hao wakimkabidhi sh. 500,000 mmoja wa wananchi wa Kwadelo walioathirika na mafuriko. Kwa mujibu wa Diwani Kariati (wapili kushoto), fedha hizo zimetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Meembe ambaye ni mzee wa heshima wa kata hiyo.
Diwani Kariati akikagua maeneo yaliyoathiriwa na mafuriko katika moja ya vijiji vya Kata ya Kwadelo, kufuatia mvua zoinazoendelea katika maeneo mbalimbali nchini
Kariati akionyeshwa maeneo yaliyoathirika
Wazee wakiomba dua ya kheri baada ya shuguli za uzindizi wa Kampnei ya kilimo kwanza na kukagua maeneo ya walioathiriwa na mafuriko: Picha na Bashir Nkoromo.
Wazee wa Kwadelo wakati wakisubiri kuwasili kwa diwani wao pamoja wasanii hao
Baadhi ya akinamama wa Kwadelo waliohudhuria hafla hiyo
Ray akipozi picha na wazee wa Kwadelo
Kariati akiwa na wasanii hao kwenye trekta kabla ya uzinduzi wa kampeni hiyo
Wema Sepetu akiungurumisha trekta ikiwa ni sehemu ya uzinduzi wa kampeni hiyo. Wapili Kulia ni Omary Kariati
Uwoya naye akilijaribu trekta kwenye uzinduzi huo
KWADELO HOYEEEEEE! JB akihamasisha wakati wakiwa kwenye trekta la kilimo katika uzinduzi huo
Treka likionyesha mfano wa ulimaji wa kisasa kwenye shamba la shule ya sekondari ya Kwadelo wakati wa uzinduzi huo
KITUKO: Panzi! Panzi! Panzi!, Wema Sepetu (shati ya kijani) akifunika uso wake kwa kipochi chake, huku akipiga kelele na kujiingiza katika kundi la wazee, kwa sababu ya kuogopa panzi aliyemdandia wakati wa shughuli za uzinduzi huo shambani.
J B na Wema wakila mapozi shambani wakati wakienda sehemu ya uzinduzi
Wema akitangaza kuzindua kampeni hiyo
BAADAYE: Wasanii hao wakimkabidhi sh. 500,000 mmoja wa wananchi wa Kwadelo walioathirika na mafuriko. Kwa mujibu wa Diwani Kariati (wapili kushoto), fedha hizo zimetolewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Bernard Meembe ambaye ni mzee wa heshima wa kata hiyo.
Diwani Kariati akikagua maeneo yaliyoathiriwa na mafuriko katika moja ya vijiji vya Kata ya Kwadelo, kufuatia mvua zoinazoendelea katika maeneo mbalimbali nchini
Kariati akionyeshwa maeneo yaliyoathirika
Wazee wakiomba dua ya kheri baada ya shuguli za uzindizi wa Kampnei ya kilimo kwanza na kukagua maeneo ya walioathiriwa na mafuriko: Picha na Bashir Nkoromo.
SERIKALI YAPANIA KUFUFUA RELI TANZANIA
1:35 PM
No comments
(PICHA NA IKULU)
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,
SERIKALI imetangaza hatua kubwa na kabambe za kufufua usafiri wa abiria na mizigo, ikiwa ni pamoja na ununuzi wa mabehewa na injini za treni, katika hatua kubwa za aina yake kuchukuliwa na Serikali kwa muda mrefu katika kurekebisha usafiri wa treni nchini.
Waziri wa Uchukuzi, Mheshimiwa Harrison George Mwakyembe ametangaza hatua hizo leo, Alhamisi, Januari 10, 2013, wakati alipokuwa anamkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete kuweka jiwe la msingi kwenye ukarabati mkubwa wa Uwanja wa Ndege wa Tabora ikiwa ni tukio la mwisho la ziara yenye mafanikio makubwa ya siku tano ya Rais Kikwete katika Mkoa wa Tabora.
Mheshimiwa Mwakyembe amemwambia Rais Kikwete na mamia kwa mamia ya wananchi waliohudhuria sherehe ya uwekaji jiwe hilo la msingi kwenye Uwanja huo kuwa Wizara yake imeanza kubadilisha reli nyepesi, iliyochakaa na yenye uzito mdogo kwa Reli ya Kati.
Amesema kuwa kwa kupitia mashirika yake ya RAHCO na Shirika la Reli Tanzania (TRL) Serikali itafanya marekebisho hayo makubwa njia mzima ya Reli ya kati na kuwa mafundi wa mashirika hayo tayari wamefika Mkoa wa Morogoro.
Waziri Mwakyembe amemwambia Rais Kikwete kuwa Serikali kupitia Wizara yake na mashirika yake hayo, imeagiza mabehewa mapya ya mizigo 274, imeagiza mabehewa mapya ya abiria 22, imeagiza mabehewa mapya ya kubebea kokoto 25 na pia imeagiza mabehewa ya breki (brake vans) 34 na tayari malipo ya awali yamefanyika.
Katika namna inayothibitisha dhamira ya Serikali kurekebisha hali ya usafiri wa reli nchini, Mheshimiwa Mwakyembe pia amewaambia wananchi kuwa Wizara yake pia imeagiza crane mpya na kubwa ya kubebea mizigo yenye uzito unaofikia kilo 100.
Kuhusu injini za treni, Waziri Mwakyembe amemwambia Rais Kikwete kuwa zabuni kwa ajili ya kutengeneza upya (re-manufacturing) injini nane za treni imetolewa ili utengenezaji huo ufanyike, iwe ni ndani ama nje ya nchi.
Pia Waziri amesema kuwa oda imetolewa kwa ajili ya utengenezaji wa injini mpya 13 za treni ambazo malipo yake yatafanyika katika mwaka ujao wa fedha hata kama utengenezaji wa injini hizo utaanza.
Aidha, Waziri amesema kuwa Wizara kupitia mashirika yake hayo mawili imeagiza spea za kutosha kuweza kufanya ukarabati mkubwa wa injini tano kwenye karakana zilizoko hapa nchini.
“Mheshimiwa Rais, kwa hesabu nyepesi tu ni kwamba katika kipindi kifupi tutaweza kuwa na injini kiasi cha 26 ambazo zitarudisha uhai wa usafiri wetu wa reli kwa kiasi kikubwa sana,”Waziri Mwakyembe amemwambia Rais Kikwete.
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
10 Januari, 2013
Monday, January 7, 2013
ZIARA YA KIKWETE IGUNGA ILIVYOTIKISA!
11:04 AM
No comments
Sunday, January 6, 2013
NGOMA MPYA YA R.O.M.A ft STORY - 2030.
2:08 PM
No comments
Anakwenda kwa jina la STORY ndiye aliyeimba CHORUS ya nyimbo mpya ya ROMA - 2030 (ILE SAUTI YA KITOTO)
|
Subscribe to:
Posts (Atom)
ZILIZOSOMWA ZAIDI
-
Mhifadhi utalii katka hifadhi ya Mlima Kilimanjaro (KINAPA),Eva Mallya akizungumza juu ya ofa iliyotangazwa na hifadhi hiyo ya kupanda m...
-
O FISI YA RAIS SEKRETARIETI YA AJIRA KATIKA UTUMISHI WAUMMA Kumb. Na EA.7/96/01/G/50 1 Agosti, 2014 TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI Sekret...
-
Send Off ya Flaviana Matata ilifanyika huko mkoani kwao, Shinyanga. Flavvy akiwa na Matron wake, Jennifer Bash Akifanyiwa makeu...
-
1. NISHA JABU 2. FLAVIANA MATATA 3. NELLY KAMWELU 4. JOKATE MWEGELO 5. NANCY SUMBELARI 6. BELINA MGENI 7. VANESSA M...






























