Friday, August 14, 2015

MABALOZI MIA MOJA WA CCM MONDULI, WAHAMIA CHADEMA

Mabalozi wa mashina miamoja na kumi wa CCM mwenyekiti katibu kata wajumbe wa kamati ya siasa ya kata pamoja na wenyeviti wa mitaa minne katika kata ya Monduli mjini mkoa Arusha wamehama CCM na kuhamia Chadema.

Tukio ilo limetokea Monduli mjini leo majira ya saa sita mchana wakati viongozi hao walipo kusanyika na kutoa kauli ya kuhama CCM na kuhamia Chadema huku wakieleza sababu zinazo wafanya kufikia maamuzi hayo.

Kwa upande wao wenyeviti wa serikali za mitaa wajumbe wa nyumba kumi na katibu wa CCM kata ya Monduli Anna Erinest wameitaka jamii itambue kuwa hayo ni maamuzi yao binafsi na hayahusiki na shinikizo la mtu yoyote kama inavyo daiwa na baadhi ya watu kila wanaohama udaiwa wameshinikizwa.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI