Monday, August 24, 2015

LOWASSA ALIPOMSINDIKIZA MAALIM SEIF SHARIFF HAMAD KUCHUKUA FOMU YA KUGOMBEA URAIS WA ZANZIBAR (UKAWA)


Mgombea Urais wa Zanzibar wa UKAWA kupitia Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad akionyesha mkoba wenye Fomu za kuwania nafasi hiyo, Agosti 23, 2015, kwenye Ukumbi wa Salama, Bwawani, Zanzibar.
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha akimkabidhi Mgombea Urais wa Zanzibar wa UKAWA kupitia Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, Fomu za kuwania nafasi hiyo, Agosti 23, 2015, kwenye Ukumbi wa Salama, Bwawani, Zanzibar.
Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa akimpongeza Mgombea Urais wa Zanzibar wa UKAWA kupitia Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, baada ya kuchukua Fomu za kuwania nafasi hiyo, Agosti 23, 2015, kwenye Ukumbi wa Salama, Bwawani, Zanzibar
Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jecha Salim Jecha akisoma taarifa ya muongozo kwa Mgombea Urais wa Zanzibar wa UKAWA kupitia Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad, wakati wa kuchukua Fomu ya kuwania nafasi hiyo, Agosti 23, 2015, kwenye Ukumbi wa Salama, Bwawani, Zanzibar. Maalim Seif alisindikizwa na Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa, Mgombea Mweza, Dkt. Juma Haji Duni pamoja na viongozi wengine wanaounda UKAWA.
Mgombea Urais wa Zanzibar wa UKAWA kupitia Chama cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) Agosti 23, 2015, kwenye Ukumbi wa Salama, Bwawani, Zanzibar. Kulia kwake ni Mgombea Urais wa Tanzania wa UKAWA kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Mh. Edward Lowassa pamoja na Mgombea Mweza wake, Dkt. Juma Haji Duni.
#CHADEMA Blog

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI