Monday, August 17, 2015

TAARIFA KUHUSU NAPE KUWEKWA PEMBENI ZAKANUSHWA

Katibu wa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye (kushoto) akiwa kwenye kikao cha Kamati Kuu Maalum leo tarehe 17 Agosti 2015, kinachoendelea kwenye Makao Makuu ya Chama,Ofisi Ndogo Lumumba.
Ndugu Msomaji, kuna taarifa za uongo zimeenezwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii zikisema kuwa Kamati kuu ya CCM imemuweka kando Katibu wa Itikadi na Uenezi Ndugu Nape Nnauye kutoka katika nafasi hiyo na kumteua Ndugu John Chiligati kushika wadhifa huo.
Taarifa hizo si za kweli kwani Kamati kuu haijafanya uamuzi wowote wenye mlengo huo.
Wahariri naomba mpuuze taarifa hizo za uzushi zenye lengo baya na zinazoandaliwa kwa makusudio maksusi.
#CCM blog

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI