Friday, March 20, 2015

MWANDISHI WA KITABU CHA MTEMI MIRAMBO, JUMA NATURE KUGOMBEA UBUNGE? NA RUBY KAANZA BIASHARA? #255 *AUDIO*

Sky WeezyFredrick Bundala ambae amekuja na kitabu kinachozungumzia maisha ya Mtemi Mirambo wa Tabora, akizungumzia kitabu hicho amesema ni  idea  iliyozoeleka nchi za nje na baada ya kupitia mitandao akagundua Audio box  kwenye soko ni kitu kikubwa sana na anapenda sana kusimulia matukio kama alivyowahi kufanya katika documentary kuhusu Mv Bukoba akaona anauweza kufanya kitu kwa kusimulia na watu wakakipenda akatengezena kitabu katika mfumo wa sauiti (Audio Box) kinachoitwa Mtemi Mirambo (Sultani Mkuu wa Afrika)
natureBaadhi ya wasanii wameonekana kuhamia kwenye siasa kama Mr TwoProf. JayAfande Sele na wengine msanii Juma Nature amesema alikuwa amepanga kufanya hivyo na watu walimfata ila mwa mkwa huu ameona asigombee, kama angegombea Ubunge Temeke angepita ila kwa sasa amewaachia wasanii wenzake, ikitokea akawa Mbunge jambo la kwanza kufanya kwa wanachi wake ni barabara ya Mbagala, Hospitali pamoja na Soko na ataingia chama chochote atakachoona kinamsingi mzuri.
Wasanii wengi wa Bongo Flava wameendelea kujiingiza kwenye biashara, 255 leo imepiga story na msanii Ruby ambae amesema anapenda kuwa designe, anatarajia kuja na kitu kinachoitwa ‘Kilemba cha Ruby’ ambayo inahusuana na mambo ya fashion, idea ambayo imekuja kutokana na kupenda kudesigne vilemba toka akiwa mdogo ingawa kipaji chake kikubwa ni kuimba.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI