Thursday, December 25, 2014

INASIKITISHA: KITENDO ALICHOFANYIWA WASTARA SI CHA KIUNGWANA

 “…Nilitukanwa sana jana kwa kuwish wenzangu kheri ya xmass na kuonekana sina dini... Niseme kitu kimoja wasanii kwenye mitandao hatupo kwa ajili ya kutangaza dini tupo kwa ajili ya kutangaza kazi zetu na kuwa karibu na nyinyi mashabiki wetu.

Pili kazi yangu hainunuliwi na watu wa dini moja tu mi nafikiri uvivu wa kufikiri na wepesi wa kusahau kuwa msanii ni nani ndio unawafanya maneno mengi yawatoke, mi msanii sio mwana zuoni msinivike taji lisilo kuwa langu, kama mahodari wa kufundisha watu dini basi katazeni na viongozi wenu wa kislam wasijumike na watu wakatazeni na kina Salmankhn wa India ambao wamemaliza misahafu lakin wanavaa kofia za xmass, Je kazi zetu zingenunuliwa kwa ajili ya dini, tungekuwa wapi leo?
Nina follows zaidi ya elfu 96 sidhani kama wote ni dini yangu, kifupi sipendi malumbano ya dini kwenye page yangu plz naheshimu kila mtu na kila shabiki yangu hata kama mpagani ukitukana tu hapa mi na wewe..” - Wastara Sajuki
Huu si uungwana jamani, udini sio ishu! Tubadilike.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI