Thursday, October 9, 2014

JIFUNZE KITU: SIMBA DUME AKICHEZEA KICHAPO KIKALI TOKA KWA KUNDI KUBWA LA NYATI *+PICHAZ*

Simba dume amejikuta katika hali tata baada ya kutolewa mkuku na Nyati katika Hifadhi ya Kruger, nchini Afrika Kusini, walipomfumania akiwa katika mawindo yake. 
Gazeti la Daily Mail la Uingereza limeripoti.
Hakika waswahili husema mbio za sakafuni huishia ukutani na za mwizi ni 40 siku yako ikifika hata uwe mtemi vipi watakukamata tu. 
Simba akitimua mbio huku akifuatwa kwa kasi na Nyati.
Nyati walimfikia na kumchota mtama wa aina yake na kukaa chini.
Simba alianza kula nyingi tu za uso kama alivyonaswa na camera ya Lyle Gregg.
Walipiga kila kona ya mwili wa Simba na kumjeruhi vibaya sehemu za kichwa.
Simba alipoteza kabisa ubabe wake maana mateke ya kichwa yalimuandama na pembe.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI