Monday, August 18, 2014

MSIBA!!! MZEE LEWIS MAKAME AFARIKI DUNIA: ALIYEKUWA KATIKA TUME YA UCHAGUZI

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji Lewis Makame.
ALIYEWAHI kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), 
Jaji Lewis Makame (pichani) amefariki dunia leo katika Hospitali ya AMI, 
Masaki jijini Dar es Salaam alilokuwa amelazwa kwa ugonjwa uliokuwa unamsumbua.
Jaji Makame ambaye kwa kipindi kirefu aliongoza NEC, alilazwa katika hospitali hiyo mwishoni mwa mwezi Julai. Rais Jakaya Kikwete alimtembelea kumjulia hali Julai 28, mwaka huu.

Kwa vipindi viwili, Jaji Makame akiwa Mwenyekiti wa NEC,  ndiye aliyetangaza matokeao ya uchaguzi Mkuu wa 2005 na 2010 ambapo Rais Kikwete aliibuka mshindi dhidi ya vyama pinzani.
Rais Dk. Jakaya Mrisho Kikwete akimjulia hali  leo, Mwenyekiti mstaafu wa Tume ya Uchaguzi Jaji Mstaafu, Lewis Makame aliyelazwa katika hospitali ya AMI iliyoko Mikocheni jijini Dar es Salaam Julai 28,2014.
Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi.
Tutaendelea kukujuza kadri tunavyozipata taarifa juu ya msiba huu.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI