Wednesday, July 30, 2014

MASTAA WANAPOJUTIA KUWA NA TATTOO KATIKA MIILI YAO *PICHAZ*

Producer Pharrell Williams alishawahi kukiri kuwa alipata maumivu makali sana wakati anafuta tattoo alizochora wakati wa ujana wake na akajutia kitendo hicho.
Alikuwa muoga wa magonjwa atakayopata baada ya tattoo kufutwa na mionzi mikali kwenye mwili wake inayoweza kusababisha saratani na magonjwa mengine.
Angelina Jolie alibidi afute tattoo ya mpenzi wake wa awali Billy Bob aliyoichora wakati wako pamoja.
Huyu ni mwigizaji Matt" Damon alijichora tattoo kabla hajawa B list Super Star wa filamu marekani na kuamua kuifuta ili kujenga heshima zaidi.
Jamaa aliweka midomo ya rapper Trina kwenye shingo yake wakati wako pamoja na baada ya kuachana nae alibidi afute tattoo, Maumivu yake sasa ndio ilikuwa shidaaaah!
Baada ya kuachana na mke wake Jennifer Lopez, Marc Anthony ilibidi afunike tattoo ya jina la Jennifer na kitu kingine. Aliogopa maumivu ya kufuta.
50 Cent kashazoea kufutwa na kuchora tattoo zingine kwenye maisha yake. Akiwa na jambo jipya huongeza tattoo anavyo jisikia

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI