Ripota
wa nguvu Albert G. Sengo kutoka Mwanza anaripoti Mmisionari Simon
Nyirani Mhagama wa Shirika la Mt. Kalorilwanga ambaye anasambaza ujumbe
kuhusu hayati Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere kuwa Mtakatifu wa
21 tangu tarehe 20/03/2013.
Picha
ya mwisho ya Hayati Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere aliyopiga
kijijini kwake Butiama kabla ya kwenda kupata matibabu nchini Uingereza
ambapo alifia katika Hospitali ya Mt. Thomas.
Wakati yote haya yakifanyika kutoka nchini Uganda: Rais Yoweri
Museveni, amesema kiongozi bora ni yule anayefuata maagizo ya Mungu na
kuwatumikia binadamu wote kwa usawa na haki.
Rais Museveni aliyasema hayo Tarehe moja mwezi June, wakati wa ibada ya kuombea mchakato wa kumfanya Marehemu Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kuwa mwenyeheri na hatimaye kutangazwa mtakatifu.
Rais Museveni aliyasema hayo Tarehe moja mwezi June, wakati wa ibada ya kuombea mchakato wa kumfanya Marehemu Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere kuwa mwenyeheri na hatimaye kutangazwa mtakatifu.
Picha
ya mchoro wa Mtakatifu Charles Lwanga aliyemtangaza Hayati Baba wa
Taifa kuwa Mtakatifu wa 21 ambapo alisema hata kwenye maandiko
matakatifu ya Biblia kuna mistari inayomtaka binadamu ampende binadamu
mwenzake kama anavyojipenda yeye.
Rais Museveni alisema anatarajia kupeleka
ushahidi kwa Papa Benedict kwamba Mwalimu Nyerere ana sifa za kutangazwa
kuwa mtakatifu kwa sababu alimtii Mungu na kuwatumikia binadamu.
Mmisionari
Simon Nyirani Mhagama wa Shirika la Mt. Kalorilwanga ambaye anasambaza
ujumbe kuhusu Hayati Baba wa Taifa Julius Kambarage Nyerere kuwa
Mtakatifu wa 21 akiwa katika picha ya pamoja na watoto waliotembelea
kaburi la Baba wa Taifa Butiama mkoani Mara.
Kufuatia hatua hiyo ya kwenda Roma kutoa ushahidi, Rais Museveni
amesema katika maadhimisho ya kuombea mchakato wa Mwalimu kuwa Mtakatifu
yatakayofanyika mwakani, ameahidi kuwaita maraisi wote waliowahi
kufanya kazi na Mwalimu Nyerere ili kuuthibitishia ulimwengu kuwa
Marehemu Baba wa Taifa ameweza kuwa unganisha Waafrika.
Alifafanua kuwa Mwalimu ametoa mchango mkubwa wa ukombozi kwa nchi za
Msumbiji, Zambia, Zimbabwe, Namibia, Angola, Afrika Kusini, Uganda na
Tanzania yenyewe. Hivyo kuja kwa viongozi hao kushiriki ibada hii
itakuwa Baraka kubwa.
Kwa kanisa katoliki utakatifu ni hatua ya tatu baada ya hatua ya
kwanza ambayo ni Mtumishi wa Mungu,hatua ya pili ni Mwenye Heri na hatua
ya tatu ni Mtakatifu ambapo miujiza mbalimbali pamoja na taarifa
hukusanywa kupelekwa makao makuu ya Kanisa hilo.
0 comments:
Post a Comment