Monday, April 14, 2014

MRADI WA SECO WAZINDULIWA MKOANI ARUSHA

Katibu Mtendaji wa UNCTAD Dk. Mukhisa Kituyi (Kushoto), Mkurugenzi wa Idara ya Mtangamano wa Biashara wa Wizara ya Viwanda na Biashara, Lucas Saronga (Katikati) na Balozi wa Uswizi nchini Olivier Chave (Kulia) wakisaini hati za makubaliano ya utekelezaji mradi wa SECO.
Picha ya pamoja ya Washiriki wote wa Mkutano na uzinduzi wa mradi wa SECO uliofanyika mjini Arusha.
Baadhi ya Washiriki wa uzinduzi wa mradi wa SECO uliofanyika Jijini Arusha.
Baadhi ya Washiriki wa uzinduzi wa mradi wa SECO uliofanyika Jijini Arusha.
MRADI wa kuunganisha sekta za Wazalishaji matunda, mbogamboga na wenye hoteli (SECO)unaofadhiliwa na Serikali ya Switzerland umezinduliwa Jijini Arusha. 
Mradi huo ambao lengo lake kuu ni kuboresha maisha ya Watanzania wanaojihusisha na sekta hizo kwa kuongeza uzalishaji wao na uhakika wa masoko ya ndani na nje yanchi, unaanza utekelezaji wake mara moja ukiwa na thamani ya jumla ya Dola za Kimarekani milioni tatu na nusu.
Uzinduzi wa Mradi huo umeshuhudiwa na Katibu Mtendaji wa UNCTAD, Dk. Mukhisa Kituyi, Balozi wa Uswizi nchini Tanzania Olivier Chave na Mkurugenzi wa Idara ya Mtangamano wa Biashara katika Wizara ya Viwanda na Biashara, Lucas Saronga.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI