Friday, March 14, 2014

RAIS DKT. KIKWETE NA VIONGOZI WA BUNGE MAALUM LA KATIBA DODOMA

D92A4568
Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mh.Samuel Sitta (kushoto) na Makamu Mwenyekiti Mhe.Samia Suluhu (kulia) wakati wa hafla  ya kuwaapisha katibu na naibu katibu wa Benge maalum la katiba zilizofanyika katika viwanja vya ikulu ndogo mjini Dodoma leo asubuhi
D92A4522Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Katibu na naibu katibu wa Bunge maalum la Katiba muda mfupi baada ya kuwaapisha katika ikulu ndogo mjini Dodoma leo asubuhi.Kushoto ni Katbu Wa Bunge hilo Bwana Yahya Khamis Hamad na kulia ni Naibu Katibu Dkt. Thomas Kashililah.
D92A4644Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na viongozi waandamizi wa serikali na viongozi wa bunge maalum la katiba muda mfupi baada ya kuwaapisha Katibu na Naibu Katibu wa Bunge hilo katika hafla iliyofanyika ikulu ndogo mjini Dodoma leo. 
Kutoka kushoto ni Katibu wa Bunge maalum la Katiba Bwana Yahya Khamis Hamad,Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Ombeni Sefue. Waziri Mkuu Mizengo Pinda, Mwenyekiti wa Bunge Maalum la Katiba Mh. Samuel Sitta,Makamu Mwenyekiti wa Bunge maalum la Katiba Mh. Samia Suluhu, Makamu wa pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Balozi Sefu Iddi, Naibu Katibu wa Bunge Maalum Dkt. Thomas Kashilila na kulia ni Mwenyekiti wa muda wa Bunge maalum la katiba aliyemaliza muda wake Mh.Pandu Ameir Kificho
(Picha na Freddy Maro).

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI