Saturday, November 7, 2015

HAFLA YA UZINDUZI WA BODI MPYA WA WAKURUGENZI WA MAMLAKA YA MAFUNZO NA AMALI

Waziri wa Elimu na mafunzo ya amali Zanzibar, Mhe Ali Juma Shamuhuna akimkabidhi cheti Dk Mohammed Hafidh Khalfan katika hafla ya kuwaaga wanabodi ya wakurugenzi wa mamlaka ya mafunzo na amali  waliomaliza muda wao na pia uzinduzi wa Bodi mpya. Hafla hii ilifanyika tarehe 05/11/2015 kwenye ukumbi wa mafunzo ya amali. Wengine waliosimama ni Katibu Mkuu na Naibu katibu Mkuu Wizara ya Ealimu na mafunzo Amali.
Mwanzoni mwa mwezi Oktoba 2015, Dk Khalfan aliteuliwa tena na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein kuendelea kuwa mwenyekiti wake kwa miaka mitatu ijayo.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI