Friday, May 1, 2015

KUTANA NA MABINTI AMBAO USTAA UMEWASHINDA BONGO MUVI!

Skaina Ally 
Wapo mabinti ambao waliingia kwenye fani ya uigizaji kwa mbwembwe, wakawika sana kwenye vyombo vya habari na kuunyemelea ustaa lakini ghafla wakayeyuka.Walipoibukia kwenye fani walionekana watakuwa tishio na kuwafunika wale wakongwe waliokuwa wakionekana wao ndiyo wao. Sasa hivi hawajulikani wako wapi na wanafanya nini. Huyu alikuwa tishio sana miaka ya nyuma.
Umbo lake tata, uzuri wake vilimbeba, akawavutia baadhi ya wanamuziki ambao walimfanya kuwa Video Queen kwenye nyimbo zao kama vile Bob Junior aliyemtumia kwenye ‘kichupa’ chake cha Wimbo wa Kimbiji.
Aliigiza kwenye filamu mbalimbali kupitia Kampuni ya RJ. Hata hivyo, baadaye aliolewa kisha akaachika, mara akabeba ujauzito uliodaiwa ni wa mwanamuziki Nay wa Mitego. Baada ya kujifungua akawa kimya, mwanaye ni mkubwa lakini haijulikani sasa anafanya nini.

Zamda Salim
Huyu naye aliibuka miaka 2010 kwenye soko la filamu. Ana umbo zuri lililomfanya atumike kwenye filamu kadhaa.
Naye alionekana kuja kuwafunika mastaa lakini cha kushangaza akaanza kufifia na mpaka sasa hata wewe msomaji unayefuatilia masuala ya burudani ukiulizwa yuko wapi na anafanya nini huwezi kuwa na jibu.
Mara ya mwisho zilivuja picha akiwa amevaa shela, watu wakasema ameolewa lakini wengine wakadai ni filamu.
Zamda Salim 

Ester Flaviana
Huyu ni mmoja wa maandagraundi walioibuka kwa kasi ya ajabu. Aling’ara kwenye magazeti, akaonekana kwenye filamu mbalimbali lakini naye mara ya mwisho zilivuja picha zake za utupu na mpaka leo hii haijulikani kajichimbia wapi.

Diana Kimaro
Diana Kimaro ni binti f’lani mcharuko. Mcharuko wake umeonekana kwenye filamu mbalimbali alizocheza kama vile Family Disaster. Aling’ara sana alipokuwa akiigiza kwenye filamu kama Pacha wa Elizabeth Michael ‘Lulu’.
Mara ya mwisho alikuwa akisoma Moshi kisha baadaye akaonekana kwenye filamu ya Msuto Daily na Kigodoro lakini hawiki kama anavyowika shoga yake Lulu.

Rehema Fabian
Aliibukia kwenye Shindano la Miss Kiswahili 2008, akapaa zaidi pale alipokuwa akitoka kwenye magazeti na skendo tofauti huku akionekana kwenye filamu mbalimbali.Mara ya mwisho alikimbilia nchini China ambapo alidai kuchumbiwa na mtoto wa kigogo wa Nigeria. Juzikati ilisemekana ni mjamzito, amekaa kimya haijajulikana anafanya nini.

Neema Chande
Huyu alitokea kwenye umiss, alivuma sana alipojiingiza kwenye masuala ya filamu na kufikia hatua ya kutoa filamu yake aliyoipa jina la Time Goes Around. Alipamba kurasa mbalimbali za magazeti kwa habari zake tofauti.
Staa huyu kwa sasa yupo nchini India, anaonekana kwenye mitandao tu ya kijamii, haijulikani anafanya nini huko lakini kwenye anga za mastaa amepotea kabisa.

Pendo wa Maisha Plus
Jina lake kamili ni Upendo Mushi. Staa huyu aliibukia kwenye Shindano la Maisha Plus. Baada ya hapo alicheza kwenye filamu mbalimbali. Kuna kipindi ilidaiwa kutoka na marehemu Kanumba na Diamond Platnumz.
Lakini naye sasa hivi haijulikani anafanya nini. Wapo wanaosema anaigiza lakini habari zake zimekuwa ngumu kuzipata tofauti na ilivyokuwa zamani ambapo alikuwa hakauki kwenye vyombo vya habari.

Amisuu Malick
Huyu naye alipamba kurasa za magazeti baada ya kuibukia kwenye umiss. Wapo wanaodai alichumbiwa ndiyo sababu ya kuwa kimya.Marafiki zake wa karibu wanasema kuwa ameamua kutulia na kufanya mambo yake ambayo si lazima yaanikwe hadharani.

Sharzy Sadry
Huyu naye ni staa ambaye alitoka na marehemu Steven Kanumba kwenye filamu ya ‘The Shock’. Alionekana kuwashtua mastaa wa Bongo kwani filamu hiyo aliicheza kwa umahiri.Wapo waliosema kuwa Kanumba alimchukua ili kuziba pengo la Wema kwani kwa wakati huo Wema na Kanumba walikuwa wameachana.

Halima Madiwa
Aliibukia kwenye uigizaji wa filamu. Waliomchezesha kwenye filamu waliamini kuwa angekuja kuwa tishio. Akawa hakauki kwenye magazeti lakini naye cha ajabu kapotea.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI