Sunday, February 1, 2015

MUME AMUUA MKEWE BAADA YA KUJIFUNGUA MTOTO WA JINSIA ASIYOITAKA *PICHAZ*

Vuysi Turan akiwa na mke wake ambaye ni Marehemu.
KWA WANANDOA wengi linapokuja suala la kupata watoto wengi wao hupanga na kuwa na matarajio mengi juu ya ujio wa watoto wanaowatarajia, lakini pia kunakuwepo na chagua la jinsia ya mtoto atakayezaliwa ambalo huamuliwa na pande zote mbili.
Lakini pia Matukio ya unyanyasaji yameendelea kuwepo baina yao hasa pale mwanaume anapotaka kitu fulani na kisifanikiwe kwa wakati huo kama ambavyo mwanaume huyu Vuysi Turan raia wa Uturuki kuamua kumuua mkewe siku moja baada ya kujifungua mtoto wa pili wa kike kitendo kilichomkasirisha baada ya kutaka mtoto wa kiume.
Aysun Sesen akiwa amembeba mtoto wa dada ake.
Turan amehukumiwa adhabu ya kifo baada ya kumpiga mkewe na shoti ya umeme kisa tu amemzalia mtoto wa kike wakati yeye alikua akitaka wa kiume.
Kwa mujibu wa mahakama iliyomuhumu mwanaumehuyo adhabu ya kifo ilieleza kuwa, mwanamke huyo baada ya kutoka hospitali kujifungua mumewe alinunua nyanya za umeme na kuziwasha kisha kumchoma nazo miguuni hadi kufariki dunia.

0 comments:

Post a Comment

ZILIZOSOMWA ZAIDI