Monday, September 1, 2014

MTU MMOJA ANUSURIKA KIFO BAADA YA GARI KUPINDUKA TEMEKE

Gari aina ya Landusider lenye nambari za usajili T540 APN lililokuwa likitokea Temeke kuelekea Tazara, Dar es salaam lilipinduka jana wakati dereva wa gari hilo alipokuwa akijaribu kulikwepa Lori lililokuwa limeegeshwa pembeni ya barabara wakati akiwa kwenye mwendo kasi.Dereva huyo alikuwa akilikimbiza gari lingine aina ya Canter moja (namba zake za usajili hazikufahamika mara moja) lililokuwa likitokea Temeke nalo likiwa na mwendo kasi, na hata baada ya gari lake kupinduka dereva huyo alitoka upesi upesi bila kuijali afya yake na kisha kuchukua bodaboda na kuendelea kuifukuza ile Canter. 
Askari Polisi akijaribu kufanya mawasiliano na wenzake wakati wa ajali hiyo,huku mashuhuda wakiwa wamelizunguka gari hilo.
Picha na Evance Ng'ingo wa Habari5blog

0 comments:

Post a Comment