TIMU ya taifa ya Afrika kusini maarufu kama Bafana bafana ambayo kwa sasa inaongoza group A imeanza vema baada ya kufanikiwa kuifunga timu ya kongo kwa jumla ya goli mbili kwa bila.
Ephraim Shakes
Kocha wa timu hiyo Ephraim Shakes anaamini kuwa timu yake inarudi katika chati baada ya ushindi huo na kwamba ana matumaini ya kuelekea Morroco 2015
Hata hivyo licha ya ushindi huo Afrika Kusini inatarajia kurudiana na Timu ya Taifa ya Congo katika mchezo unaotarajia kufanyika katika uwanja wa Peter Mokaba ulioko mjini Polokwane mapema Oktober 15 mwaka huu mchezo ambao utaamua kama timu hiyo itashiriki fainali za mataifa ya Afrika nchini Morroco.
Kihistoria timu hizi zimekutana mara tisa huku Bafana bafana ikiwa imeshinda mara tano na kupoteza mara moja.
No comments:
Post a Comment